Saturday, September 24, 2016

ZIFAHAMU ATHARI HIZI ZA WHATSAPP, FACEBOOK, INSTAGRAM KATIKA MAHUSIANO


Faida za WhatsApp , Facebook,  Instagram au mitandao mingine ya kijamii unazijua ? Au kufupisha habari je, wewe unanufaika na hii mitandao ya kijamii ?  Kutana na bwana M, ambaye anadai kwake faida kubwa ya mitandao hii ni kuwa inamfanya asijione mpweke.  Ni sehemu  ya burudani na kufahamu nini kinaendelea katika ulimwengu unaomzunguka.

Anachozungumzia bwana M ni kuwa mitandao  ya kijamii kama WhatsApp , Facebook , na Instagram inawapa watu wengi uwezo wa kujielezea yale ambayo pengine katika mazingira waliyopo wanashindwa kujieleza.

Athari za Uhuru wa kujieleza ndani ya WhatsApp, Facebook , Instagram
Hata hivyo hapo katika kujielezea ndipo kunapoweza leta matatizo badala ya kumsaidia mtumiaji wa mtandao. Nazungumzia pale ambapo mtu badala ya kukaa chini na mhusika na kumueleza malalamiko yako, wewe unatoka na kuenda kutangaza matatizo yako au kutoridhika kwako au hasira zako huko mtandaoni.

Status/Posts za WhatsApp, Facebook, Instagram zinasema mengi
Kuna watu unaweza jua mood zao kupitia status wanazoweka. Kwa yule ambayo amekukosea au mliye katika mfarakano, yeye hatojisikia vizuri hata kidogo, na huko unapoenda kutangaza wala hakuna wa kukusaidia.

Tafsiri ya posts zako za WhatsApp, Facebook, Instagram
Jambo lingine la kukumbuka ni kuwa kama unapopost malalamiko, kashfa au kejeli kwa kuwa umekasirishwa au unahisi kuonewa na mtu fulani , unajijengea picha mbaya kwa baadhi ya watu kuwa wewe si mzuri katika mahusiano ya mtu na mtu, hivyo watu wakae mbali nawe , kwani hujui namna ya kumaliza matatizo kati yako na watu unaohusiana nao, badala yake unakimbilia mtandaoni.
Athari zake

Unapojionyesha kuwa hauna uwezo wa kumaliza matatizo yako bila kuenda mtandaoni , unajiweka katika mazingira magumu mfano ya kupata kazi, au kupata washirika wa kufanya nao dili za biashara n.k kwakuwa wataogopa kuaibishwa mtandaoni.

Pia kujizoesha kukimbilia mtandaoni kutangaza matatizo yako badala ya kutafuta njia ya kuyamaliza huko pembeni , kunadhoofisha uwezo wako wa kujenga mahusiano bora.
Hitimisho

Pamoja na umuhimu wa mitandao ya jamii ya kutuweka karibu na watu wengi, tusisahau kujenga mahusiano ya mtu mmoja mmoja. Na lolote linalotokea baina yako na mtu au kundi fulani huko nje ya mitandao ya kijamii, jitahidi ulimalize huko huko nje, na sio kulipeleka mtandaoni kana kwamba huko mtandaoni kuna majaji wa kukupatia haki.

Monday, September 19, 2016

ORODHA YA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA UFUNDI KWA MWAKA 2016

Tumia namba ya shule, jina la mwanafunzi au shule atokayo kurahisisha kupata shule aliyochaguliwa mwanafunzi

1

Tuesday, September 13, 2016

UTAJUAJE KAMA UNA UPUNGUFU WA MAJI MWILINI?


Umeshawahi kwenda hospitali kumlalamikia daktari kuwa mwili wako hauna nguvu na unajisikia kuchokachoka sana na baada ya kukuchunguza, akakwambia huna tatizo lolote isipokuwa una upungufu wa maji mwilini tu?

Mwili kuishiwa nguvu huwa ni miongoni mwa dalili za upungufu wa maji mwilini na chanzo kikiwa ni wewe mwenyewe kutopenda kunywa maji. Ni kawaida kwa baadhi ya watu kutokunywa maji hadi pale wanaposikia kiu.

Katika makala ya leo, nitakujuza dalili za mwili kuishiwa maji ambazo hujitokeza na kukuhimiza kunywa maji hata kabla hujasikia kiu. Uonapo dalili hizo, hupaswi kuzipuuzia bali kunywa maji kwa wingi tena haraka.

UPUNGUFU WA MAJI MWILINI NI NINI?
Pale mwili unapopoteza kiasi kingi cha maji kwa njia mbalimbali, ikiwemo jasho na mkojo, mwili hupungukiwa maji na hivyo mtu huyo huambiwa ana upungufu wa maji. Tunaelezwa kuwa karibu theluthi mbili ya miili yetu imejaa maji.

Ili mwili uweze kufanya kazi yake vizuri, kiwango cha maji mwilini hakipaswi kupungua hata kidogo, hivyo kila mtu ana wajibu wa kunywa maji ya kutosha kila siku ili kulinda kiwago chake cha maji kisipungue na kinapopungua ndipo hapo mwili huanza kuonesha dalili za kukaukiwa maji (dehydration).

NINI HUSABABISHA?
Sababu zinazosabababisha mwili kukaukiwa maji huweza kuwa nyingi, lakini zinazojulikana zaidi ni pamoja na:
Kuacha kunywa maji
Kukaa kwenye joto kwa muda mrefu
Kunywa kiwango kikubwa cha pombe,
Ungonjwa wa kisukari ambao husababisha mtu kukojoa mara kwa mara
Kutokwa na jasho jingi, kwa sababu ya ama kufanya kazi ngumu au mazoezi. Hivyo inashauriwa mtu anayetokwa jasho jingi kunywa maji mara kwa mara wakati akiendelea na shughuli inayomtoa jasho.
Kama ukiugua au ukipatwa na homa kali, huweza kupungukiwa na maji mwilini
Kutapika na kuharisha nako huweza kupoteza maji mwilini.

DALILI ZA KUKAUKIWA MAJI KWA WATOTO
Kwa kawaida, dalili za upungufu wa maji mwilini hujitokeza zaidi kwa watoto wadogo kuliko watu wazima au wazee. Dalili za upungufu wa maji mwilini kwa watoto huweza kusabababishwa ama na kuharisha, kutapika, kutokunywa maji au vimiminika vingine vya kutosha.
Mtoto mwenye dalili za upungufu wa maji huweza kuonesha dalili zifutazo:

Kukojoa mara chache sana
Mtoto kutokuwa mchangamfu
Macho, tumbo au mashavu kubonyea
Mdomo na ulimi kukauka
Mtoto kulia mara kwa mara na anapolia machozi hayatoki.

DALILI ZA UPUNGUFU WA MAJI KWA WAZEE
Dalili za upungufu wa maji kwa wazee ni tofauti na watu wazima. Wazee wa umri zaidi ya miaka 60 huwa na ngozi iliyosinyaa na hata ukiiminya, hubaki katika hali hiyo kwa muda na unapoikwaruza alama hubaki.

Halikadhalika, wazee hukosa haja ndogo kwa muda mrefu, hupungukiwa uzito kwa kiasi kikubwa na hupatwa na homa.

DALILI ZA UPUNGUFU WA MAJI KWA WAJA WAZITO
Upungufu wa maji mwilini kwa waja wazito ni hatari kwa mama pamoja na mtoto. Dalili zinazoweza kujitokeza kwa waja wazito ni pamoja na:

Kukojoa mkojo wa njano nyeusi
Kuumwa na kichwa
Mwili kukosa nguvu
Kichefuchefu na kutapika
Kukaukwa na mdomo

Ili kujiepusha na matatizo ya upungufu wa maji na hatimaye kujikuta unakumbwa na dalili kadhaa zilizoelezewa hapo, ambazo ziko pia kwa watu wazima wengine, ni kuwa na mazoea ya kunywa maji ya kutosha kila siku. Hata utakapozidiwa na kukimbizwa hospitali, hakuna dawa nyingine utakayopewa zaidi ya maji (re-hydrating solution). Kwa nini usubiri hali hiyo ikutokee wakati unaweza kuizuia kwa kunywa maji tu

Umuhimu Wa Mawasiliano Katika Kujenga Mahusiano Bora Ya Kijami


Habari rafiki na mpenzi msomaji wa Amka Mtanzania? Natumaini unaendelea vema katika kuboresha maisha yako na karibu katika makala yetu ya leo.

Katika dunia ya leo mawasiliano ni kitu muhimu sana katika maisha yetu. Mawasiliano ndio yanatuwezesha mimi na wewe kuweza kuwasiliana na kupashana habari katika makala hii. Huwezi kupata huduma yoyote bila mawasiliano. Mawasiliano bora ndio yanamuwezesha mtu kupata kazi au huduma nzuri kwa urahisi. Makampuni ya simu yanatumia lugha ya ushawishi ili kuweza kukuvuta wewe kama wangetumia lugha mbaya yaani mawasiliano mabovu wasingeweza kukushawishi.

Mawasiliano mazuri na watu ndio yanakupa au kukuhakikishia kupata fursa nzuri kwa watu. Watu wanashindwa kufanikiwa katika mambo mengi ni kwa sababu tu ya kutokuwa na mawasiliano mazuri na kukosa lugha ya ushawishi. Unaweza kuwa na kitu kizuri lakini jinsi unavyokiwasilisha kwa lugha ya hovyo nao watu watakuchukulia siyo mtu makini. Mafanikio tunayoyatafuta yanapatikana kwa watu hivyo ni lazima uwe na mawasiliano mazuri na mahusiano mazuri na watu. Pia inabidi kutumia mawasiliano sahihi kulingana na sehemu na mtu au watu husika. Unapokuwa unawasiliana na watu tumia lugha rasmi na siyo lugha ya mtaani kwani lugha rasmi inakutambulisha kuwa wewe ni mtu makini na watu watakuheshimu na kujenga imani na wewe.

Epuka mawasiliano yanayoweza kuwagawa watu kulingana na itikadi za kiimani tumia mawasiliano bora ambayo yanaweza kutumika kwa mtu yoyote yule bila kumgawa kinamna yoyote ile. Na tofautisha watu, mtu, kundi, taasisi, kampuni, rafiki, mpenzi katika mawasiliano.

Mawasiliano katika biashara; katika biashara mawasiliano bora na huduma bora ndio yanayoweza kumshawishi mteja wako. Mteja anahitaji lugha nzuri ya ushawishi na siyo kumlazimisha. Lugha mbaya ni kero na inaweza kusababisha kumpoteza mteja. Kama mfanyabiashara tumia lugha nzuri ya ushawishi itakayomvutia mteja wako hata kama alikuwa hana mpango wa kununua atanunua tu kulingana na lugha nzuri ya ushawishi na ukarimu wa mtoa huduma.
Katika biashara epuka tabia ya kumsalimia mtu kwa lugha isiyo rasmi acha mazoea kabisa ukimsalimia mtu katika lugha ya mtaani yaani lugha isiyo rasmi atakuoana na wewe siyo mtu makini katika kazi yako. Katika salamu msalimu mtu habari yako ndugu, habari ya kazi nk. Ile salamu rasmi na siyo unakwenda kuwasilisha biashara yako unawasalimu watu niaje, shwari nk. Lugha hizi siyo rasmi zinakufanya uonekane siyo makini. Kwa hiyo katika biashara tumia lugha rasmi yeye ushawishi na siyo lugha ya mtaani.

Kama unajua jina la mteja wako basi muite jina lake kwani mtu anafarijika sana anapoitwa jina lake halisi na tena kwa ufasaha. Muite mtu jina lile analopenda kama anapenda umuite jina analopenda muite. Epuka kukatisha jina la mtu kama unaweza kumuita jina zima muite atafarijika zaidi. Usisahau kusema asante kwa mteja na kama unawasiliana naye kwa email, simu nk usitumie vifupi utaonekana hauko makini na hujakua kwa mfano unaandika xaxa badala ya sasa huo ni utoto waachie watu ambao wako katika hatua ya ukuaji na siyo wewe. Vivyo hivyo, tumia lugha rasmi katika maswala ya kiofisi.

Katika mahusiano; tofautisha unawasiliana na nani; mpenzi wako, rafiki yako, ndugu, jamaa na marafiki. Katika mahusiano ya kimapenzi epuka kitu kinachoitwa mazoea kwani watu waliokuwa katika mahusiano ya kimapenzi kama mke na mume huwa wanajisahau sana katika mawasiliano. Unapomtumia mwenza wako ujumbe lazima utofautishe na ujumbe unaomtumia rafiki yako. Watu wanaua mahusiano yao kwa kukosa mawasiliano mazuri mfano mtu anamtumia mpenzi wake ujumbe kama vile anamtumia rafiki bila hata kuweka vionjo mbalimbali vya kimahaba vitakavyompa faraja na upendo. Unapomtumia jumbe zilizokosa vionjo akipata mtu anayemwekea vionjo katika jumbe itakuletea dosari katika mahusiano yako kama mwenzako ameweza kuweka vionjo kwa kutumia muda wake na wewe unamtumia ujumbe mkavu kwani utapungukiwa nini ukituma kama yeye alivyotuma. Kwa hiyo, ni vema kuepuka mazoea katika mawasiliano kwani mazoea katika mawasiliano ndiyo yanavunja mahusiano.

Mahusiano ya kirafiki; unapomsalimu rafiki ni vizuri zaidi kumwita jina lake na mwisho wa mawasiliano sema asante au kama ni ujumbe wa kimaandishi andika asante mwishoni mwa jumbe yako kwa kufanya hivyo unakuwa unathamini muda wake kwa kusoma ujumbe wako, epuka vifupi vya kijinga kwani vifupi vimekuwa ni kero kwa sasa mtu anakuandikia xalamu badala ya salamu, xaxa badala ya sasa ukimuona mtu anakuandikia hivi ujue bado hajakua yuko katika hatua za ukuaji. Mtu makini hawezi kuandika vifupi. Pendelea kutumia lugha ya mawasiliano iliyo rasmi kwani itakusaidia kuonekana mtu makini katika mambo yako kuliko lugha za mtaani.

Mawasiliano lazima yawe na mrejesho yaani feedback, sasa mtu anapokusalimu kwa njia yoyote ile ya kupasa umpe mrejesho na siyo kukaa kimya tu. Mawasiliano yoyote yana gharama kuna gharama za muda, pesa, nguvu nk, hivyo mtu anapokusalimu ujue ametumia gharama hivyo basi unapaswa kuthamini salamu au mawasiliano. Mawasiliano mazuri ni yale yenye mrejesho. Kuna maneno muhimu sana katika mawasiliano kama vile samahani, asante, naomba na nk. Neno asante ni neno dogo lakini lina maana au uzito mkubwa sana linampa mtu hamasa juu ya kitu fulani. Sema asante mtu anapokupatia kitu siyo kukaa kimya.

Kwa hiyo, mawasiliano ni kitu muhimu sana, maisha ni mawasiliano ya kila siku kwani mahitaji yetu mengi ya kila siku tunayapata kwa njia ya mawasiliano. Kuna watu wanakosa kazi kwa sababu ya lugha mbaya au mawasiliano mfano mtu anapoenda katika usaili anatakiwa kutumia lugha rasmi na mawasiliano mazuri ili aweze kuwashawishi na kupata ajira. Mwingine anakwenda katika ofisi za watu na kuwasalimia watu kihuni au anakwenda mbele ya kadamnasi anawasalimu watu kihuni mfano oya niaje salamu kama hizi ni kero kwa watu na katika kundi la watu ujue kuna watu wa aina mbalimbali hivyo ni lazima utambue itifaki za watu na kuzizingatia. Hivyo unaweza kuwa na shida ukakosa kusaidiwa na watu kukupuuza kulingana na lugha au mawasiliano mabovu uliyotumia.

Mwisho, tumia mbinu bora za mawasiliano ili kujenga mahusiano bora na watu waliokuzunguka. Kama mtu anawasiliana na wewe kwa lugha ya Kiswahili usimjibu kwa kingereza.

Friday, September 9, 2016

Mambo 10 Ambayo Mwanaume Hupenda Kusikia Toka Kwa Mpenzi Wake..


10. Kukosolewa – “I think you are wrong”

Wanaume wanaweza kujikweza sana lakini daima hawachukii kurekebishwa. Wanachojali zaidi ni jinsi gani au njia gani imetumika kuwarekebisha. Mwanaume akikosea, anataka mpenzi wake amkosea lakini kwa mapenzi, sio kwa mikwaruzano au dharau au mbele ya kadamnasi. Mrekebishe au mkemee faragha, toa maoni yako na wala usimlazimishe, itamfanya aone unajali na unataka kumjenga.

9. Kujali – “How was your day?”

Wanawake wengi hutaka wao tu ndio waulizwe kuhusu jinsi siku zao zilivyoenda kila siku, wanasahau kabisa hata wanaume nao walikua kwenye mihangaiko. Mzoeshe kumuuliza mpenzi wako siku yake ilikuwaje? utaona hata nuru ya mapenzi yenu itang’aa na mtakua marafiki, japo mwanzoni atakua hakuambii kila kitu lakini baada ya muda atazoea. Kila mtu anataka wa kumsikiliza, mtu atakayezungumza nae chochote kilichotokea ndani ya siku yake, na pengine kukuuliza ushauri.

8. Ucha Mungu – “Can we pray?”

Mwanaume, anayesali au kutosali, lazima huwa ana imani kwamba Mungu yupo. Mwanamke mcha Mungu siku zote huwa ni wazo la kila mwanaume endapo ana mpango wa kuoa. Mwanaume huwa na amani kwa kiasi fulani akiongozwa na mwanamke wake kwa upande huo wa sala.

7.  Msamaha – “I forgive you”

Vikombe kwenye sahani havikosi kugongana, vivyo hivyo na kwa wapenzi, kuumizana hisia hakuepukiki, iwe kwa makusudi au bahati mbaya, mwenzio akikosea sasa isiwe ndo adhabu, akiomba msamaha ukamwambia nimekusamehe na kweli umemsamehe, funika kurasa endeleeni na maisha. Usililete tena mezani jambo ulilosema umesamehe.

6. Sifa – “That was great sex”

Kama amefanya kazi nzuri, mwambie. Wote tunajua sio kila siku watu hufanya kiwango che Maradona au Pele, siku akiwa kwenye kiwango hicho hata yeye anajua, usisite kumpa sifa zake. Wazungu wanasema, ‘Yes, you can kiss and tell some of the times’. Na kama unaona kuna sehemu anahitaji kujisogeza, mwambie pia, tena kimahaba. Hii itawasaida nyote.

5. Upekee  – “I admire you. No other man is like you”

Ni kweli kwamba kuna wanaume ambao ni wazuri na wenye uwezo mkubwa zaidi ya huyo ulienaye, lakini kwake hujisikia vyema zaidi ukimwona yeye ni zaidi ya wote hao. Sio mbele ya macho yake tu, matendo yako na hata nyuma yake msifie kwamba yeye ndio mwanaume pekee duniani unayempenda na hakuna mwingine zaidi yake.

4. Uaminifu – “I trust you”

Mwanaume akijua anaaminika sana kwa mwanamke, na yeye hujiachia. Na kwa hili huwa anaweza kugombana na watu kabisa kwa ajili ya mwanamke wake. Japo wengine hulitumia hili kwa uchafu wao lakini wengi wao ni kitu chema kwao.

3. Mapenzi –  “Make love to me”

Ni mtazamo wa wengi kwamba mwanaume ndio siku zote awe mwanzilishi wa tendo. Lakini mwanaume kwa wakati mwingine hupenda mwanamke wake ampe vishawishi na yeye vya kumleta kwenye mood. Sio kila siku aanze yeye tu, wakati tendo ni la kuwafurahisha wote. Hata kama ni ngumu kusema kwa mwanamke, ishara kibao zipo za kumuonyesha mwenzi wako akaona ‘Leo baby anataka na yeye’.

2. Malengo -“What’s your dream?”

Mwanaume anaweza asionyeshe kama anahitaji msaada, lakini kwa kutumia njia za mapenzi, unakuta ni mwanaume tu anayehitaji uwepo  wa mwanamke anayempenda yeye. Mungu alimtengeneza mwanaume na kumpatia msaidizi kwa kumpatia mwanamke. Kuwa mwanamke mwenye msimamo na mpangilio mahiri usiotikisika, ambaye unauwezo wa kumuuliza anaenda wapi katika maisha yake, na akakukumbusha huko siko ni huku. Ndoto za mwanaume mara nyingi huendana na zile na mwenzi wake, na mwanamke huwa pale kuhakikisha ndoto za pamoja zinatimia.

1. Upendo wa dhati – “I love you”

Wanaume wengi hujiona wagumu kwenye kutamka neno ‘I love you’ kwa wanawake zao na hata akisema itakua ni mara chache chache hata kama kweli kutoka moyoni wanapenda, lakini haina maana hawataki kuambiwa na watu wanaowapenda, hii huwaaminishia nafasi yao kwenye moyo wa mwanamke.