Saturday, August 27, 2016

Heart touching love story


Girl: How much do you love me?

Boy: Look up at the sky.

Girl: Don't change the subject!

Boy: Just do it!

Girl: Alright! What am I looking at?

Boy: Count how many stars there are.

Girl: Impossible.
Boy: So that is explaining how much I love you.MAMBO YA MAPENZI NI HATAR,

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya Agosti 28




ust 28, 2016 Askari Magereza Atiwa Mbaroni Kwa Kuingia Wodini Akiwa Amelewa na Kisha Kuanza Kufyatua Risasi




POLISI mkoani Rukwa inamshikilia askari Magereza, Cleophas Chapaulinge kwa kosa la kulewa na kupiga risasi hewani akiwa wodini katika Hospitali ya Mkoa wa Rukwa mjini Sumbawanga na kusababisha taharuki kubwa kwa wagonjwa na wauguzi.

Kitendo cha askari huyo kilizua taharuki kubwa kwenye wodi namba tisa ya wanawake na watoto, ambapo akinamama walipiga mayowe kwa hofu huku wakikimbia na kujificha kwenye chumba cha muuguzi wa zamu wakiwaacha watoto wao vitandani.

Akizungumza  kwa njia ya simu, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, George Kyando alithibitisha kutokea kwa tukio hilo  na kueleza kuwa lilitokea jana alfajiri.

“Chanzo ni ulevi wa kupindukia tulimpima kipimo kikaonesha kiwango cha ulevi kilikuwa juu kupita kiasi alama zikiwa 300 huku kiwango cha kawaida cha kipimo ni alama kati ya 70 na 40 …. Katika tukio hilo hakuna aliyejeruhiwa na bunduki yake ilikuwa na risasi 10,” alisema.

Kamanda Kyando alisema siku ya tukio, askari huyo akiwa na mwenzake walikuwa kwenye lindo akilinda makazi ya Kamanda wa Magereza wa Mkoa, lakini alitoroka lindo na kwenda hospitalini wodi namba tisa, ambako mkewe alikuwa akimuuguza mwanawe aliyekuwa amelazwa hapo kwa matibabu.

Mke wa mtuhumiwa huyo, Theresia Kalonga ambaye naye ni askari Magereza, alikuwa amelazwa na mtoto wao wa kike mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi 10.

“Mtuhumiwa huyo tunamshikilia huku taratibu za kumkabidhi kwa Kamanda wa Magereza Mkoa wa Rukwa ili aweze kushtakiwa kwa taratibu za jeshi lao kabla ya kufikishwa kwenye mahakama za kiraia, zinaendelea,” alisisitiza Kamanda Kyando.

Akizungumza hospitalini hapo, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Dk John Gurisha alisema askari huyo baada ya kuingia wodini, aliweka silaha yake chini akafunua chandarua na kuanza kuzungumza na mwanawe, kisha katoka nje na kufyatua risasi hewani na kutoboa paa.

“Mtuhumiwa huyo alizua kizaazaa kwani askari wetu waliokuwa lindo hapa hospitalini walilazimika kukimbia ili kuokoa maisha yao baada ya kusikia mlio huo wa risasi na kumuona askari huyo akielekea walipokuwa wamekaa,” alisema na kuongeza kuwa askari huyo aliletwa hospitalini hapo na mwendesha bodaboda ingawa hakuna mtu yeyote aliyejeruhiwa, lakini alisababisha taharuki kubwa hospitalini.

“Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) waliwahi kufika hospitalini hapo na kumtia nguvuni, na bunduki yake ilipokaguliwa ilikutwa ikiwa na risasi kumi,” alisema.

Muuguzi wa zamu wodini humo, Rose Katabi alisema askari huyo alipofyatua risasi akinamama wodini humo walianza kupiga mayowe ya kuomba msaada huku wakikimbia na kuwaacha watoto wao vitandani na kuvamia chumba cha muuguzi kwa ajili ya kusalimisha maisha yao.

“Kwanza kitendo cha kumuona askari huyo akiwa na silaha mkononi, mwili wangu wote ulikufa ganzi nilihisi atatulipua kwa kutupiga risasi za moto …aliiweka silaha yake hiyo chini na kuanza kuzungumza na mwanawe. Aliniuliza kama mtoto wake ameshakunywa dawa, nikamjibu anakunywa dawa mara moja usiku.

“Waliingia walinzi wetu wawili wodini ndipo akaanza, kusema atarudi tena, akatoka nje akiwa katikati ya mlango wa wodini alikoki bunduki yake na kufyatua risasi hewani iliyotoboa paa kisha akaondoka na kutokomea gizani,” alisema.

Kwa upande wa mke wa mshtakiwa huyo, Theresia alisema alipomuona na sare za jeshi na silaha mkononi alimtaka arudi mara moja kazini. 
Walinzi waliokuwa kwenye lindo katika lango kuu la kuingia hospitalini hapo kwa masharti ya kutoandikwa majina yao , walidai kuwa askari huyo alifikishwa hospitalini hapo kwa usafiri wa bodaboda.

“Alitutia shaka baada ya kukataa kusimama, kwani alipitiliza moja kwa moja akiwa na silaha mkononi, tulijawa na hofu kubwa tukaamua kumfuata kwa nyuma hadi akaingia wodi namba tisa alikolazwa mkewe na mtoto wake. Lakini tulipomuona akikoki bunduki yake tulilazimika kukimbia na kwenda kujificha ndipo tukasikia mlio wa risasi,” alisema mmoja wao.

Waziri Mkuu: Tanzania Iko Tayari Kujifunza Kutoka Nchi Nyingine



WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Tanzania iko tayari kujifunza kutoka kwa nchi nyingine ambazo ni wanachama wa Mpango wa Kujitathmni Kiutawala Bora barani Afrika (APRM) ili iweze kuboresha hatua ilizofikia kwenye mpango huo.

Ametoa kauli hiyo jana jioni (Ijumaa, Agosti 26, 2016) wakati akichangia mada katika Mkutano wa 25 wa Wakuu wa Nchi wanachama wa Mpango wa Kujitathmni Kiutawala Bora barani Afrika (APRM Forum) uliofanyika kwenye hoteli ya InterContinental jijini Nairobi, Kenya.

“Nitumie fursa hii kukiarifu kikao chako kwamba Tanzania imeshaanza kutekeleza mpango kazi wa Kitaifa ambao umejikita kutatua changamoto katika sekta za maji, elimu, kilimo, nishati na miundombinu kama zilivyoainishwa kwenye kikao cha APRM,” alisema.

“Ili kuhakikisha kuwa zinafanyiwa kazi haraka, changamoto hizi za kisekta zimepewa kipaumbele kwenye Mpango wetu wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa miaka mitano wa 2016-2021 ambao umejikita zaidi kwenye viwanda,” aliongeza.

Tanzania ilifanyiwa tathmini yake Januari, 2013 kwenye kikao cha Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika kilichofanyika Addis Ababa, Ethiopia.

Mapema, akifungua mkutano huo, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya alisema viongozi wa Afrika hawana budi kukubaliana na kuungana kutafuta suluhisho katika ushindani wa kibiashara.

Alisema nchi wanachama wa mpango huo hawana budi kujenga umoja kama njia ya muafaka ya kufikia makubaliano hayo.

Wakati huohuo, Rais Yoweri Museveni wa Uganda alisema bara la Afrika linakabiliwa na changamoto 11 (strategic bottlenecks) ambazo zinakwamisha maendeleo ya bara hilo na akataka zitafutiwe ufumbuzi ili kuzisaidia nchi nyingi barani humo. 

Akiwasilisha mada binafsi katika mkutano huo, Rais Museveni alisema kwa zaidi ya miaka 50, amekuwa kiongozi katika sehemu kadhaa na kwamba amebaini kuwa changamoto hizo zimezuia ukuaji wa uchumi barani Afrika pamoja na mabadiliko ya kiuchumi na kijamii.
 
Alisema asilimia kubwa ya changamoto hizo haikupata ufumbuzi hata wakati malengo ya maendeleo ya milenia (MDGs) yalipokuwa yanatekelezwa.

Alizitaja changamoto hizo kuwa ni mikanganyiko ya kiitikadi ambayo huzaa ubinafsi na maslahi binafsi; kuwepo kwa mataifa dhaifu (weak states); nguvukazi duni (kitaaluma na kiafya), uduni wa miundombinu (barabara, maji, umeme, tehama) ambao unashindwa kuvutia uwekezaji; uhaba wa viwanda unaolazimisha nchi kusafirisha mali ghafi na uhaba wa masoko ya bidhaa zinazozalishwa barani Afrika.

Changamoto nyingine ni uduni wa huduma za kijamii unaosababisha huduma mbovu kwenye maeneo ya utalii, mabenki na mahoteli; kilimo duni kisichotumia mbolea, dawa za kuua wadudu, mbegu za kisasa au njia za umwagiliaji; makosa ya kisera kama vile ubinafishaji au utaifishaji mali zinazomilikiwa na sekta binafsi; ukandamijazi wa demokrasia na ukosefu wa maadili miongoni mwa watumishi wa umma.

Naye Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini alisema kwa vile changamoto hizo zinagusa nchi nyingi za Afrika, ni vema iundwe timu ya wataalamu watakazipitia zote na kuainisha zipi zinafaa kufanyiwa kazi na kisha taarifa yao iwasilishwe kwenye kikao kijacho cha Wakuu wa Nchi wanachama.

Akifunga mkutano huo, Rais Kenyatta aliitaka sekretarieti ya APRM ipitie changaoto hizo na kuziwakilisha kwenye kikao chao kijacho ambacho alisema kitafanyika Januari 2017, mjini Addis Ababa, Ethiopia katika tarehe itakayopangwa baadaye. 
 
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAMOSI, AGOSTI 27, 2016.

Wednesday, August 24, 2016

Minister hails Aga Khan Hospital expansion.


The Minister for Health, Community Development,
 Gender, Elderly and Children, Ms Ummy Mwalimu
TANZANIA will save 25 billion/- per year from transferring patients to overseas upon completion of a major expansion of the Aga Khan Hospital that will see the health facility develop into a major teaching and tertiary academic medical centre.
The Minister for Health, Community Development, Gender, Elderly and Children, Ms Ummy Mwalimu, said in Dar es Salaam yesterday that the government spends enormous amount of money every year in providing tertiary level treatment to Tanzanians in overseas hospitals.
“The expansion will allow us to ensure that Tanzanians receive advanced medical care at home with all the convenience and support that they rightly deserve,” said the Minister at a ceremony to unveil the project.
The project worth 167bn/-, which will be commissioned by 2018, will allow the 175-beds hospital to provide best health care in non-communicable diseases. Ms Mwalimu, who was the guest of honour at the event, expressed gratitude to the Aga Khan Health Services Institution which owns the Aga Khan hospitals, for its contribution in development of health services in the country.
“The new project is truly a significant investment towards health sector public partnership investment,” she said.
Ms Mwalimu observed that the non-communicable diseases were on increase pointing out junk foods and lifestyle changes as the main cause of the diseases. Chair of the Board Executive Committee of Aga Khan Health Services, Princess Zahra Aga Khan, said her institution came up with the idea of expanding the hospital in Dar es Salaam following the increase of cases of non-communicable diseases.
“Five per cent of the cases the Aga Khan Hospitals receive are of non-communicable diseases,” she said.
Director of Projects and Clinical Programmes Development at the Aga Khan Health Services, Dr Zeenat Sulaiman, said the health facility will house clinical units of neurosciences, cancer, oncology, gynaecology and neonatology. “The health facility will have teaching and learning spaces at each clinical unit throughout the hospital for allied health professionals,” she said.
Meanwhile, Ms Mwalimu has directed Muhimbili National Hospital (MNH) Board of Directors to oversee that the hospital reduces unnecessary referrals abroad to cut government spending on the area. She also directed the board to look through the possibility that 25 per cent of medical drugs reimbursement is used for procuring medicines from the Medical Stores Department (MSD).
Ms Mwalimu made the directives when inaugurating the new MNH Board of Directors in Dar es Salaam yesterday.
"Over 25bn/- is spent on referrals outside the country every year; I am convinced that you are going to reduce the number once MNH achieves its status of a super specialist medical centre in the country," said Ms Mwalimu.
These can only be achieved by availing those health services that are sought outside the country yet they can be obtained within the country, although to some extent that has been attained citing an example of cochlear implant.
"The procurement of drugs and medical equipments at MNH should be properly scrutinized so that 25 per cent revenues obtained from medicines is used to buy the same from MSD," she said.
Ms Mwalimu called on the board to see through that collection of revenues at the hospital is improved while exercising the National health Policy for women, children under five and elderly obtain medical services freely.
"I commend MNH for a notable achievement on revenue collection from the former 2bn/- to currently 4bn/- in a month," noted the Minister. The Chairman of the MNH Board, Prof Charles Majinge, pointed out that for a long time, the performance of the hospital was not as expected due to financial constraints and lack of enough medical supplies but it was time to exercise a new vision.
"My Board will work to see that we are generating effective solutions that will work on the long existing challenges that have been facing the hospital," pointed out Prof Majinge.
All these will be achieved by MNH reflecting its status of a super speciality medical centre and improved services offered at the hospital. Meanwhile, Muhimbili National Hospital has received three ambulances from the Government of Japan and Bango Sangho Dar es Salaam.
Speaking at the handover ceremony, the Ambassador of Japan, Mr Masaharu Yoshida, said a grant contract was signed in February 2015 by the two countries, whereby Japan extended 36,603 US dollars, which is equivalent to 80m/- for the purchase of two ambulances.
‘‘Before the project, MNH had only one ambulance functioning, patience was required to use public transport or private cars for referrals, which is a big burden, particularly to the low-income people,’’ he remarked.
He added: “The situation caused delay of medical care or sometimes death of people, so upon the request of the former Executive Director, Dr Marina Njelekela, the Government of Japan decided to extend this grant," said Mr Yoshida.
On her part, Ms Mwalimu extended recognition to Japan and Bango Sangho Dar es Salaam for their assistance, noting that the ambulances will help save many lives. She called on more individuals with the ability to offer emergency service aid such as ambulances to do so to help save lives.