Monday, April 11, 2016

Jamii yatakiwa kuwasaidia watoto wa mitaani kupata elimu.


Jamii imetakiwa kuwa na moyo wa kuwasaidia watoto wamitaani kwa kuwapatia mahitaji muhimu ikiwa pamoja na kuwashawishi kuwenda shule, kwa kufanya hivyo taifa baadaye litakuwa limepunguza idadi kubwa ya vijana ambao watakuwa hawana shuguli maalumu za kufanya ikiwemo wanojihusisha na vitendo vya uhalifu.
Hayo amesema mkuu wa kituo cha kulelea watoto wa mitaani cha Chrildren Community Center cha mjini Singida Sister Sara Emmanuel baada ya viongozi wa shirikisho la wanafunzi wa vyuo vikuu mkoani Singida kutoa msaada kwa watoto hao zaidi ya miatano ambao wanalelewa na kituo hicho.
 
Akitoa msaada huo mwenyekiti wa shirikisho hilo Bi Mary Mpoke amesema wanafunzi wameguswa na kuwaonea huruma watoto hao ambao ni viongozi wa baadaye na kuamua kuwa changia kutoka katika posho zao za kujikimu chuoni na kwa kuwanunulia mikate, vifaa vya usafi, sabauni, madaftari. 
 
Kituo hicho ambacho kipo Singida mjini kimekuwa kikitoa msaada kwa kuwapatia chakula na mahitaji mengine ya shule kila siku wanapotoka shuleni kwa mashariti ya kuonyesha walicho soma kwa siku, kikiwa na  lengo la kuwa shawishi kuendelea na masomo kwa kwenda shule badala ya kuzurura na kuwa watoto wa chokoraa.
 

No comments:

Post a Comment