Saturday, January 30, 2016

Ali Kiba Amfananisha Mwanamuziki Ruby na Mbwa..Ruby Amshukia Ali Kiba na Kufunguka Makubwa

Mwanamuziki Ruby amefunguka kwa uchungu kuhusu Mwanamuziki Ali Kiba Kumfananisha na Mbwa....
"Kabla ya yote naombeni sana mashabiki zangu, mniwie radhi kwa nnacho kiandikia katika ujumbe huu binafsi mimi sijapendezewa kabisa na alichokisema kaka yangu @officialalikiba kwenye kipindi cha @thesporahshow kilichorushwa kupitia @cloudstv kaka yangu alikiba mimi ni mdogo sana kwako si kwa umri wa kimuziki, sikutegemea na sijapendezwa na kauli yako yakunifananisha mimi na MBWA mimi ni binaadam na ni mdogo wako kama alivyo @zabibu92kiba sidhani kama ungeweza kumwita huyo mbwa wako zabibu au abdul, mimi sina ukaribu wowote na wewe lakini kama mtu niliyemkuta kwenye industry na uliyenitangulia kuliona jua na mpaka uliponifwata kuniambia una- appreciate kazi yangu nakuniomba nifanye nyimbo na mdogo wako @officialbdukiba na nikakubali yote hayo yalifanikiwa kutokana na love niliyokuwa nayo kwako kama kaka yangu,hujawahi hata siku moja kunitamkia kwamba unambwa wako anaitwa Ruby, kwa sababu mimi na wewe tumesha kutana nakuongea si chini ya mara moja, hujawahi kusema hilo kwangu, ila umekuwa ukiniambia tu naimba vizurii, je ulisahau nini kaka yangu hadi kushindwa kuniambia muhusika wa jina la mbwa wako mpya,mimi nimeona ni kejeli na dharau kubwa na hazisaidii katika maisha zaidi ni kujishushia heshima yako haipendezi kwa mtu kama wewe ambae pia unaangaliwa na watu wengi kama kioo cha jamii,nategemea kuona mfano mzuri kutoka kwako nikiwa kama mdogo wako lakini umenitia giza machoni @officialalikiba kakaangu kwakweli nimekwazika sana kwasababu mimi ndo kwanza naanza game naanza kazi ya kuendeleza nchi hii na afrika kwa dunia nzima kwenye upande wasanaa ambao wewe umeshaanza muda ,lakini nimestaajabu unanifananisha na mbwa ,cha ajabu zaidi hata watu wako wa karibu @rehemavisuallab @zabibu92kiba hawaitamki wala kuileta katika jamii kwa usahihi wa mbwa kweli ,Naamini Mungu hamtupi mja wake, chozi la mnyonge haliendi bure, Me namuachia Mungu" Rubby

No comments:

Post a Comment