Thursday, January 21, 2016

Bomu lalipuka ndani ya gari mgahawani -Somalia


Maafisa wa polisi Mjini Mogadishu wameripoti kuwa Bomu lililotegwa ndani ya gari limelipuka nje ya mgahawa mmoja uliopo katika ufukwe wa bahari katika mji mkuu wa Somalia .
Masuhuda wamesema kuwa gari hilo lililojaa vilipuzi liligonga mgahawa huo maarufu wa Lido Beach kabla ya watu watano kujitokeza na kuanza kufyatua risasi.
Lido beach ni moja ya Mgahawa uliopo pembezoni mwa Mogadishu na huwavutia maelfu ya vijana wa Somalia kwenda kujipumzisha na kujifurahisha.
Jeshi la polisi kupitia kwa Meja Abdiqadir Ali limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na bado haijajulikana kama kuna waliojeruhiwa na shambulizi hilo, pia uchunguzi bado unaendelea kuwabaini waliohusika.
Chanzo BBC

No comments:

Post a Comment